Sunday, March 30, 2014

Watu wawili wamefariki dunia papo hapo na wengine kumi na mmoja kujeruhiwa vibaya wakati wakifanya kibarua cha kushusha nguzo za kusambazia nishati ya umeme vijijini kupitia kampuni ya moja  ya Derm katika kijijini cha Bisumwa wilayani Butiama mkoani Mara.
Baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo  wamesema tukio hilo limeokea leo saa 3.30 asubuhi katika kijiji cha Bisumwa wilayani Butiama,ambapo vibarua hao kutoka kijiji cha sabasaba baada ya kufika kijijini hapo na lori  hilo aina ya Scania yenye namba za usajili T 787 CUL  wakiwa juu ya sheena hiyo ya nguzo na wakati wajaribu kufungua mikanda kwa ajili ya kuzishusha nguzo hizo zilishuka kwa kasi kubwa sambamba na wao hatua ambayo imesababisha watu wawili kufariki dunia kwa kugongwa na nguzo hizo huku wengine wakipata majeraha makubwa yakiwemo ya kuvunjika kwa miguu.
Viongozi wa halmashauri ya Butiama wakiongozwa na mwenyekiti wake Bw Magina Magesa, ambao walifika muda mfupi baada ya tukio hilo kutokea kwa ajili ya kutoa msaada kwa majeruhi hao,pamoja na kutoa pole  lakini wametaka kampuni zinazohusika kusambaza nishati ya umeme katika vijiji vya mkoa wa Mara kuchukua tahadhari wakati wa kusafirisha nguzo hizo ili kuepuka ajali mbaya kama hiyo.
Kaimu kamanda wa polisi wa polisi mkoa wa Mara kamishina msaidizi wa jeshi la polisi Paul Kasabago, akizungumza na ITV kwa njia ya simu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuwataja marehemu kuwa ni Masui Magibo (20) na Salabanze John (22) wote wakazi wa kijiji cha Sabasaba wilayani Butiama na kwamba majeruhi wote wamelazwa katika hospitali ya mkoa wa Mara mjini Musoma kwa ajili ya matibabu zaidi.

0 comments:

Post a Comment

Click here

Click here

Popular Posts