|  | 
| Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu. | 
MMOJA wa wajomba wa Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu, Jacob Temu 
amekamatwa na Polisi kwa tuhuma za kumtishia maisha mlimbwende huyo. 
Tukio la kukamatwa kwa Jacob lilikuja baada ya kutishia kumuua kwa 
maneno Hoyce pamoja na shangazi yake ambaye ni Hilda Temu, katika 
mabishano ya wanaukoo juu ya sehemu ya kumzika ndugu yao, marehemu 
Emmanuel Nambuo Temu (33).
Hoyce aliliambia gazeti hili kuwa alitishiwa maisha kwa maneno wakati
 wa kikao cha wanaukoo kilichofanyika katika viwanja vya baa ya Rose 
Garden kujadili ni wapi pa kumzika marehemu Emmanuel, aliyefariki dunia 
jijini Dar Februari 16, 2014. Wakati baadhi ya wanafamilia na wosia wa 
marehemu wakitaka azikwe walipozikwa bibi na babu yake, Jacob alipinga 
hali iliyosababisha Hilda kufungua kesi katika Mahakama ya Wilaya ya 
Temeke. Jacob alikamatwa na polisi baada ya kufunguliwa jalada yenye 
kumbukumbu na OB/RB/3554/2O14 KUTISHIA KUUA ambapo kesi hiyo iko katika 
Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar. 
Katika kesi aliyoifungua Hilda na kusikilizwa hukumu kutolewa Jumatano iliyopita, Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Temeke, Kassim Sapi Mkwawa aliamuru mwili wa Emmanuel uzikwe katika shamba la mjomba wa marehemu Dk. Mercezederc Nambuo Temu ambaye ni kiongozi wa ukoo katika Kijiji cha Kitahie, mkoani Kilimanjaro. Awali kesi hiyo ya madai namba saba ya mwaka 2014, ilifunguliwa mahakamani hapo na Hilda Lewi Nambuo Temu, ambaye ni mama mzazi wa marehemu, akitaka mazishi ya mwanaye Emmanuel yafanyike Kijiji cha Kitahie Old Moshi mkoani Kilimanjaro lakini Jacob alipinga. Hakimu Mkwawa wakati wa kutoa hukumu hiyo alisema:
 
Katika kesi aliyoifungua Hilda na kusikilizwa hukumu kutolewa Jumatano iliyopita, Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Temeke, Kassim Sapi Mkwawa aliamuru mwili wa Emmanuel uzikwe katika shamba la mjomba wa marehemu Dk. Mercezederc Nambuo Temu ambaye ni kiongozi wa ukoo katika Kijiji cha Kitahie, mkoani Kilimanjaro. Awali kesi hiyo ya madai namba saba ya mwaka 2014, ilifunguliwa mahakamani hapo na Hilda Lewi Nambuo Temu, ambaye ni mama mzazi wa marehemu, akitaka mazishi ya mwanaye Emmanuel yafanyike Kijiji cha Kitahie Old Moshi mkoani Kilimanjaro lakini Jacob alipinga. Hakimu Mkwawa wakati wa kutoa hukumu hiyo alisema:
“Baada ya kupitia maelezo ya pande zote mbili nimebaini kuwa pande 
zote mbili za ndugu wanachobishana si Kijiji cha Kitarara wala Kitahie 
bali hawataki marehemu azikwe kwenye shamba la ukoo. “Lakini kwa kuwa 
baba mkubwa wa marehemu Dk Mercezederc amekubali marehemu Emmanuel 
azikwe kando ya shamba lake lililopo Kitahie, hakuna aliyepoteza baina 
ya pande zote mbili, hivyo marehemu akazikwe hapo,” alisema hakimu na 
akasema gharama za kesi kila upande ujibebee. Kutokana na h






 9:43 PM
9:43 PM


 
 
 
 
 

0 comments:
Post a Comment